Page 43 - Kiswahili Grade 5 Yaliyomo ya kidijitali
P. 43

10.  Kudhibiti Itikadi za



                     Kidini na za Kijamii




               Mlango 19. Matumaini ya Ivoni

               Mlango 20. Dhehebu la Ajabu

               Kusikiliza na kuzungumza

               Tashbihi za tabia
               1.   Mwenye bidii kama mchwa au nyuki

               2.   Mtundu kama tumbili
               3.   Mzembe kama kupe au chaza au kozi

               4.   Mjinga kama samaki
               5.   Mjanja kama sungura au Abunuasi

               6.   Mkali kama simbabuka
               7.   Mwoga kama kunguru
               8.   Mnafiki kama panya au ndumakuwili

               9.   Mwenye maneno mengi kama chiriku
               10.  Mnyamavu kama kaburi au mava

               11.  Wazi kama mchana
               12.  Mwenye huzuni kama mfiwa

               13.  Tulia kama maji mtungini
               14.  Furahi kama mama aliyepata mtoto salama

               15.  Hasira kama za mkizi
               16.  Mpole kama kondoo
               17.  Kuwa n wasiwasi kama kuku mgeni au mwasi

               18.  Mwenye inda au uchoyo kama joka la mdimu
               19.  Kuiga kama kasuku

               20. Mwenye maringo kama tausi
               21.  Tumainia kama tai

               22. Mvumilivu kama mtumwa
               23. Mlafi kama fisi

               24. Mwaminifu kama njiwa
   38   39   40   41   42   43   44   45   46   47   48