Page 42 - Kiswahili Grade 5 Yaliyomo ya kidijitali
P. 42

Mara kwa mara, magonjwa husababisha migogoro
               katika jamii. Baadhi ya wagonjwa kwa mfano, wanaougua
               msongo wa mawazo, wasiposhughulikiwa vyema huweza

               kuzua fujo.
                   Magonjwa mengine husababisha watu na mataifa
               yawe maskini. Mfano mzuri ni ugonjwa wa Virusi vya
               Korona. Kuanzia mwishoni mwa 2019, ugonjwa huu
               ulienea haraka katika sehemu nyingi za dunia. Safari

               nyingi za ndege, treni, magari na meli zilisimamishwa.
               Michezo na mikutano mingi pia ilisimamishwa. Biashara
               nyingi pia zilifungwa. Huu ni ugonjwa ulioletea watu
               wengi umaskini mkubwa.
                   Jambo la kuhuzunisha zaidi ni kuwa, mara kwa mara,
               magonjwa husababisha vifo. Hii huonyesha wazi kuwa
               magonjwa ni adui mkubwa. Tunafaa tujikinge dhidi
               ya magonjwa. Yanapotokea, tunafaa kuyashughulikia

               ifaavyo.
   37   38   39   40   41   42   43   44   45   46   47