Page 41 - Kiswahili Grade 5 Yaliyomo ya kidijitali
P. 41

vyetu vidogo maji na kuelekea kiamboni.

                   Jioni baada ya kula kilalio, niliamua kumweleza
               shangazi mawazo yangu. Nilimwambia kuhusu hatari
               ya vyakula na vitafunio alivyozoea kutuletea. Vilevile,
               nilimwambia kuhusu hatari za kufulia nguo mtoni.
               Shangazi Rukia alinisikiliza kwa makini. Baadaye,
               alinishukuru kwa ushauri wangu.

                   “Huenda ndiyo sababu mimi na watoto wangu, mara
               nyingi, huugua. Mara, mafua, mara kukohoa na mara
               kuhara na kutapika,” shangazi aliniambia.
                   Nilipowatembelea tena likizo iliyofuata, mambo

               yalikuwa tofauti. Shangazi aliniambia kuwa matatizo yao
               ya kiafya yalikuwa yameisha. Hata majirani zao walikuwa
               wameacha mazoea ya kufulia nguo mtoni.
               Matini 2

                                       Madhara ya magonjwa
























                   Magonjwa ni adui mkubwa wa maendeleo. Magonjwa
               husababisha pesa nyingi kutumika katika gharama za
               matibabu. Isitoshe, mgonjwa hushindwa kutekeleza
               majukumu yake vizuri. Hali hii huleta umaskini. Kwa
               mfano, mfanyakazi akiwa mgonjwa, hawezi kufanya kazi
               zake ipasavyo. Vivyo hivyo, mwanafunzi akiwa mgonjwa,
               hataweza kuyamudu masomo ifaavyo. Ukweli ni kuwa,
               umaskini una maafa mengi katika jamii.
   36   37   38   39   40   41   42   43   44   45   46