Page 40 - Kiswahili Grade 5 Yaliyomo ya kidijitali
P. 40

9. Magonjwa







               Mlango 17. Kinga ni Bora kuliko Tiba

               Mlango 18. Afya Bora kuliko Mali

               Kusoma

               Kusoma kwa mapana

               Soma matini yafuatayo.
               Matini 1
                                            Mwamko mpya


















                   Naikumbuka likizo ya Desemba mwaka uliopita.
               Nilienda kumtembelea shangazi Rukia. Shangazi alikuwa
               mwanabiashara sokoni. Alikuwa na wana wawili:
               msichana wa miaka minne na mvulana wa miaka mitano.
               Alikuwa akituletea keki, peremende, biskuti na soda kila
               jioni. Mara nyingine, alituachia asubuhi pesa za kununulia
               chipsi na juisi katika kibanda kilichokuwa karibu na
               kwake.

                   Wakoi wangu walifurahia maisha hayo lakini mimi
               sikuyafurahia. Shangazi hakuwa akienda kazini siku za
               wikendi. Sote tuliandamana na shangazi hadi mtoni
               Jumamosi moja. Alikuwa amebeba tita la nguo. Alizifulia
               nguo hizo mtoni. Majirani wake pia walikuwa wakizifulia
               nguo mtoni.

                   Shangazi alizianika nguo kando ya mto ili zikauke.
               Zilipokauka, tulimsaidia kuzianua kisha tukavijaza vibuyu
   35   36   37   38   39   40   41   42   43   44   45