Page 46 - Kiswahili Grade 5 Yaliyomo ya kidijitali
P. 46

Miezi michache baadaye, mambo yalianza kubadilika.
               Watoto wa Mzee Kosi walianza kukosa kuhudhuria
               masomo siku za Jumatatu na Jumanne. Aliwatetea kwa

               kusema kuwa walihitaji kupumzika baada ya maombi na
               shughuli nyingi za Jumapili. Mwalimu mkuu aliwaita Mzee
               Kosi na mkewe shuleni na kuwashauri kutotatiza masomo
               ya wana wao.
                   Baada ya miezi kadhaa, watoto wa Mzee Kosi walikosa
               kufika shuleni kabisa. Mwalimu mkuu na walimu wa
               madarasa ya watoto wale walienda nyumbani kwa Mzee

               Kosi kuchunguza kiini. Waliwashawishi na kuwashauri
               wazazi wale kuwaruhusu watoto wasome. Mambo
               yalipogonga mwamba, walipiga ripoti kwa chifu wa eneo
               lao.
                   Chifu alifika nyumbani kwa Mzee Kosi. Alipigwa
               na butwaa. Maskini watoto wa Mzee Kosi walikuwa
               wamefungiwa chumbani! Walikuwa wakikariri vifungu
               vya maneno kutoka kitabu fulani cha kidini. Chifu alitaka
               kujua ni kwa nini watoto wale hawakwenda shuleni.
                   “Imani yetu haituruhusu kufanya hivyo,” Mzee Kosi

               alimwambia chifu.
                   “Hamuoni mnawanyima haki ya elimu watoto hawa
               kwa kisingizio cha imani?” Chifu alichemka.
                   Mzee Kosi na mkewe hawakuwa na maneno ya
               kujitetea.

                   Chifu alihakikisha watoto wa Mzee Kosi wamerudishwa
               shuleni. Mzee Kosi na mkewe walipewa ushauri nasaha.
               Mwishowe, walitoka gizani na kutupilia mbali mafunzo ya
               dhehebu hilo la ajabu.
   41   42   43   44   45   46   47   48