Page 44 - Kiswahili Grade 5 Yaliyomo ya kidijitali
P. 44

Kusoma

               Kusoma kwa mapana
               Matini ya kidijitali

               Soma matini yafuatayo.
               Matini 1

                                            Matumaini ya Ivoni

























                   “Miaka mitano sasa na mtoto hazungumzi! Ama
               amerogwa au amelaaniwa!” Mzee Igoko alimfokea
               mkewe.
                   “Baba Ivoni, usiseme hivyo. Ivoni alizaliwa na ulemavu
               wa ubongo,” mkewe Igoko alijibu.

                   Mamake Ivoni alijua mapema kwamba mwana wao
               alikuwa amepooza ubongo. Juhudi zake za kumtafutia
               msaada wa kiafya ziligonga mwamba. Ukali wa mumewe
               ulimjaza hofu. Alikuwa ameonywa dhidi ya kumtoa
               nje. Mumewe alisema kwamba watu wangewacheka
               wangegundua kwamba mwanao wa miaka mitano
               hakuwa akizungumza. Basi maisha ya Ivoni yakawa ni
               humo tu ndani ya chumba cha ndani.

                   Majirani hawakuwahi kumwona mtoto huyo kwa
               miaka hiyo mitano ijapokuwa walisikia kilio chake kila
               siku. Hakikuwa kilio kama cha watoto wengine. Hali hiyo
               ndiyo iliwafanya wachukue hatua.
   39   40   41   42   43   44   45   46   47   48