Page 45 - Kiswahili Grade 5 Yaliyomo ya kidijitali
P. 45

Asubuhi moja, Mzee Igoko na mkewe walitokewa na
               wageni; maafisa wa watoto wakifuatwa na majirani.
               Wageni hawa walitaka kumwona mtoto aliyefungiwa

               katika chumba cha ndani. Hiyo ndiyo siku maisha ya Ivoni
               yalipata matumaini.
                   Maafisa wa watoto na wa afya waliwapongeza
               majirani kwa kupiga ripoti. Hata hivyo, walisikitika
               kwamba iliwachukua muda mrefu kufanya hivyo.

                   “Mkisikia jambo kama hili tena, chukueni hatua mara
               moja ili kuwaokoa mapema watoto kama hawa,” afisa
               mmoja wa watoto aliwaambia majirani.
                   Katika siku kadhaa zilizofuata, maafisa wa watoto na

               wa afya walihakikisha kwamba Mzee Igoko na wazazi
               wengine kama yeye wameelewa kwamba ulemavu
               wanaozaliwa nao watoto hausababishwi na laana wala
               uchawi. Ulemavu huo hutokana na matatizo ya kiafya
               yanayofaa kushughulikiwa na wataalamu wa afya ya
               watoto.

               Matini 2
                                           Dhehebu la ajabu





















                   Kila mkazi wa kijiji cha Petu alimjua Mzee Kosi. Mzee
               Kosi alikuwa na mke na watoto wanne. Kwa miaka mingi,
               alikuwa muumini wa dhehebu moja pale kijijini. Hata
               hivyo, alilihama dhehebu hilo na kujiunga na dhehebu
               tofauti karibu na mji wa Kuseko.
   40   41   42   43   44   45   46   47   48