Page 37 - Kiswahili Grade 5 Yaliyomo ya kidijitali
P. 37

Miti husafisha hewa. Miti hutoa hewa ya oksijeni
               ambayo viumbe huitumia. Jamani, kupuuza  kuitunza miti
               ni sawa na kujiangamiza!

                   Halikadhalika, miti hutupatia vyakula na matunda.
               Vyakula na matunda hustawisha maisha. Chanzo kikubwa
               cha vyakula vyetu ni miti.

                   Nani asiyejua kuwa baadhi ya miti hutupatia dawa?
               Dawa nyingi za kutibia watu na mifugo hutokana na miti.
               Mfano mzuri ni mti wa mwarobaini.
                   Miti hutupatia bidhaa nyingi tunazozitumia
               katika maisha ya kila siku. Hata vitabu na madaftari
               tunayoyatumia yametokana na miti. Je, samani

               unazozitumia shuleni na nyumbani zimetokana na nini?
               Vilevile, miti hutumika katika ujenzi.
                   Miti ina faida tele. Tunafaa kuipanda kwa wingi na
               kuitunza. Hatuna budi kuepuka kukata miti kiholela.
               Aidha, shughuli nyinginezo zinazochangia uharibifu wa
               miti zinafaa kukomeshwa.



               Sarufi
               Umoja na wingi wa nomino za ngeli ya KU-KU

               Sikiliza nomino za ngeli ya KU-KU zikisomwa.







                       Umoja                              Wingi

                1.     kusoma                             kusoma

                2.     kucheza                            kucheza
                3.     kulala                             kulala

                4.     kusimama                           kusimama

                5.     kulima                             kulima

                6.     kuandika                           kuandika
   32   33   34   35   36   37   38   39   40   41   42