Page 36 - Kiswahili Grade 5 Yaliyomo ya kidijitali
P. 36

6.   Hupendelea kutembea kutoka nyumbani hadi shuleni.

               7.   Mimi hupanda mimea na kuinyunyizia maji.
               8.  Mimi huwasaidia wazazi wangu kupambanua taka
                   kwani kila aina inaweza kutumiwa kwa namna tofauti.
                   Kwa mfano, baadhi ya taka zinaweza kutumiwa

                   kama mbolea, nyingine zinaweza kulishwa mifugo na
                   nyingine zinaweza kutengenezwa upya kwa mfano,
                   chupa za plastiki.
               Ukipata nafasi, nawe nieleze mambo unayoyafanya huko
               kijijini.


               Wasalimie wote.

               Mwenzako,

               Titokawa.


               Kuandika
               Insha ya maelezo

               Kielelezo cha insha ya maelezo




                                               MITI NI UHAI
                   Miti ina faida chungu nzima. Bila miti, sidhani
               kungekuwa na maisha ya watu na wanyama. Ukweli ni
               kuwa, miti ni uhai.

                   Miti huvuta mvua. Majani ya miti huchangia kutungika
               kwa mawingu ya mvua. Ukataji miti unaweza kuchangia
               kuadimika kwa miti kama maziwa ya kuku.
                   Isitoshe, miti huzuia mmomonyoko wa udongo. Mizizi
               ya miti hushikilia udongo ili usibebwe na maji na upepo.
               Mbali na hayo, majani ya miti hukinga udongo hutokana

               na kupigwa moja kwa moja na matone ya mvua. Miti
               pia hupunguza kasi ya upepo jambo ambalo pia huzuia
               mmomonyoko wa udongo.
   31   32   33   34   35   36   37   38   39   40   41