Page 35 - Kiswahili Grade 5 Yaliyomo ya kidijitali
P. 35

Tulipakiwa ndani ya lori siku moja na kusafirishwa
               hadi kiwandani. Humo, tulikatwakatwa zaidi. Tulioshwa
               kisha tukayeyushwa na kutengenezwa upya. Wengine

               wetu tulitumiwa kutengeneza fulana. Wengine
               tukatengenezewa chupa zingine. Wapo waliotengenezewa
               mifuko ya kulalia. Vifuniko vyetu vilitengenezewa
               miswaki.
                   Bado niko dukani mwa kuuzia nguo nikisubiri

               kununuliwa. Sijui nitafikishwa wapi. Hata hivyo,
               natekeleza wajibu wangu wa kujenga taifa.
               Mkiwa wawiwawili, fanyeni shughuli hizi.
               1.   Je, wewe hutupa wapi chupa za plastiki unazozitumia?

                   Mweleze mwenzako.
               2.   Je, wewe hutumiaje chupa za plastiki baada ya
                   kuzitumia? Mweleze mwenzako.

               Matini 3


               Kutoka kwa: titokawa@gmail.com
               Mada: Naipenda dunia

               Mpendwa Wematenda,

               Unaendeleaje?

               Ninakuandikia kukujuza kuwa yapo mambo kadhaa
               ambayo mimi huyafanya ili dunia iwe bora. Mambo haya
               ni kama yafuatavyo.
               1.   Mimi huzima taa za stima nikitoka chumbani na
                   nikienda kulala.

               2.   Mimi huepuka kutumia maji visivyo.
               3.   Mimi huzitupa taka kwenye biwi wala sizitupi
                   ovyoovyo.

               4.   Mimi huwalisha ndege ambao huishi karibu na
                   nyumba yetu.

               5.   Mimi hutumia pande mbili za karatasi ninapochora au
                   kuandika.
   30   31   32   33   34   35   36   37   38   39   40