Page 33 - Kiswahili Grade 5 Yaliyomo ya kidijitali
P. 33

Nyuki nao walifika. Walimwambia kuwa walinuia
               kufanya makao yao hapo. Baadaye, twiga walifika na
               kumwomba Mzee Saka asiukate mti huo kwa sababu

               walitegemea majani yake kwa chakula.
                   Mwanawe Mzee Saka alifika na kumwomba asiukate
               mti huo kwa kuwa mara, kwa mara, ulitoa maua ya
               kupendeza. Mkewe Mzee Saka alifika pia. Alimwomba
               mumewe asiukate mti huo kwa kuwa aliyatumia kama

               kuni matawi yake yalipokauka na kuanguka.
                   Jirani wa Mzee Saka alifika na kumkumbusha kuwa,
               mara nyingi, waliketi kivulini mwa mti huo na kupiga
               soga. Kwa nini aukate? Jirani mwingine alifika na
               kumkumbusha Mzee Saka kwamba alipokuwa mgonjwa,
               alimchemshia majani ya mti huo na kuyatumia maji hayo
               kama dawa. Pia alimkumbusha kuwa aliweza kukata
               matawi ya mti huo na kuyatumia kutengeneza nyumba

               yake.
                   Mzee Saka alizinduka kutoka usingizini. Alishangazwa
               na ndoto yake. Uchovu ulikuwa umeisha. Hewa ya hapo
               chini ya mti ilikuwa safi. Ilipendeza ajabu. Mzee Saka
               aliokota vifaa vyake na kurudi nyumbani. Baadaye, alirudi

               na mbolea na kuitandaza shinani mwa mti huo.
               Fanyeni shughuli hizi katika vikundi.
               1.   Kwa zamu, simulianeni kisa mlichokisoma kwa ufupi.

               2.   Mmejifunza nini kutokana na kisa mlichokisoma.
                   Elezeaneni.
               3.   Tambueni faida za miti zinazojitokeza katika kisa hiki.
   28   29   30   31   32   33   34   35   36   37   38