Page 32 - Kiswahili Grade 5 Yaliyomo ya kidijitali
P. 32

7. Elimu ya Mazingira






               Mlango 13. Kosa Langu Mjini

               Mlango 14. Mkulima Darasani


               Kusoma
               Kusoma kwa mapana

               Soma matini yafuatayo.
               Matini 1
                                         Ndoto ya Mzee Saka

























                   Hapo zamani, aliishi mzee mmoja aliyeitwa Saka.
               Nyumba ya mzee huyo ilikuwa karibu na msitu. Siku moja,
               alichukua shoka na upanga na kuelekea msituni. Alinuia
               kuukata mti mmoja uliokuwa karibu na nyumba yake.

                   Alianza kuukata mti shinani. Mti huo ulikuwa na
               shina pana. Aliendelea kukata hadi akachoka. Aliketi
               kupumzika. Kutokana na uchovu, alishikwa na usingizi
               mzito. Alipokuwa usingizini, aliota ndoto ya ajabu. Ndege
               walikuwa wakija sikioni mwake. Walimwomba asiukate

               mti huo kwa kuwa walijenga viota vyao kwenye matawi
               yake. Nyani nao walikuja wakamlilia asiendelee kuukata
               mti huo. Walimwambia kuwa waliishi kwenye mti huo na
               hata kula matunda yake.
   27   28   29   30   31   32   33   34   35   36   37