Page 34 - Kiswahili Grade 5 Yaliyomo ya kidijitali
P. 34

Matini 2

                             Maisha yangu kama chupa ya plastiki


















                   Tulitengenezewa kiwandani; mimi na ndugu zangu.

               Ndugu zangu walichukuliwa na kutiwa juisi. Wengine
               walitiwa soda. Mimi nilitiwa maji safi ya kunywa.
               Nilibebwa na kupelekwa hadi dukani. Nilikaa dukani kwa
               siku chache. Nilinunuliwa na mteja mmoja siku moja.
               Punde, alinifungua na kuyanywa maji yote.
                   Nilidhani angenitupa kwenye biwi la taka. Hakufanya
               hivyo. Alinibeba hadi kwake nyumbani. Alinitia maji
               mengine aliyoyanyunyizia maua yake.

                   Siku moja, kulikuwa na sherehe nyumbani kwa mtu
               huyo. Mtu huyo alikata maua na kuyaweka mdomoni
               mwangu na kuipamba meza yake. Sherehe zilipoisha,
               aliyatupa maua yale. Watoto wake walinichukua na
               kunikata vipande viwili. Nusu ya chini walinitia mchanga

               na kunipandia mmea. Nusu ya juu walinitengeneza na
               kuzipanga kalamu zao ndani yangu.
                   Baada ya miezi michache, mmea uliondolewa na
               kupandwa shambani. Nami nilitupwa jaani. Hata sehemu
               yangu iliyokuwa ikiwekwa kalamu ilitupwa pia. Mtu
               mmoja aliyebeba gunia aliniokota. Alinipeleka katika stoo
               yake. Tulikuwa wengi humo. Tulikuwa tumekatwakatwa,
               kupondwa na kuchafuliwa.
   29   30   31   32   33   34   35   36   37   38   39