Page 29 - Kiswahili Grade 5 Yaliyomo ya kidijitali
P. 29

“Yeye atasafiri hadi kituo cha mwisho cha garimoshi.”

                   “Safari yangu haitaishia hapo,” mzee alisema.
                   “Unasafiri hadi wapi?” Mwuzatiketi alimwuliza.

                   “Je, ni nani atanitetea siku ya kiama mbele ya
               Muumba kwa kosa la kutolipia kifurushi changu? Hili
               ni garimoshi la umma na kila mtu anastahili kufuata
               sheria na kulipa nauli inayofaa bila mapendeleo.” Mzee
               alimwambia mwuzatiketi huku akimpa pesa za tiketi ya
               kifurushi.

               Mkiwa wawiliwawili, fanyeni shughuli hizi.
               1.   Je, ungekuwa mzee huyo, ungefanya nini? Mweleze
                   mwenzako.

               2.   Mwambie mwenzako umejifunza nini kutokana na
                   hadithi hii.

               Matini 3
                                           Fadhila za punda

















                   Zamani sana, aliishi mfanyabiashara mmoja. Alifanya
               biashara ya kununua na kuuza chumvi. Alimtumia punda

               wake kubeba chumvi hiyo. Alimtunza vizuri. Kumbe
               fadhila za punda huyo zilikuwa mashuzi!
                   Siku moja, punda huyo alipokuwa na mzigo wa chumvi
               mgongoni, aliteleza na kuanguka mtoni. Mwanabiashara
               alifanya haraka na kumtoa punda wake mtoni.

                   Punda aligundua mzigo wake ulikuwa mwepesi.
               Alifurahi sana. Chumvi nyingi ilikuwa imeyeyuka majini.
   24   25   26   27   28   29   30   31   32   33   34