Page 27 - Kiswahili Grade 5 Yaliyomo ya kidijitali
P. 27

Kusoma

               Kusoma kwa mapana: matini

               Soma matini yafuatayo.
               Matini 1
                                    Kisa cha Mtema na Malaika




















                   Hapo zamani aliishi mtemakuni aliyeitwa Mtema.
               Mtema alitumia shoka lake kupasua magogo ya kuni.
               Alijipatia riziki kwa kazi hii. Licha ya kazi yake, Mtema
               aliwahimiza wanakijiji wenzake kupanda miti kwa wingi.
               Hata yeye alipanda miti mingi kila msimu wa mvua.

                   Siku moja alikuwa akipasua gogo kando ya mto. Shoka
               lake la chuma lilichomoka kutoka kwenye mpini wake
               na kutumbukia mtoni. Mtema alilitafuta bila mafanikio.
               Alimwomba Mola ili amsaidie.
                   Ghafla bin vuu, Malaika alitokea.

                    “Je, unatafuta nini ndugu?” Malaika alimwuliza
               Mtema.
                   “Natafuta shoka langu. Limetumbukia mtoni kwa
               bahati mbaya,” Mtema alimjibu.

                   Malaika alitumbukiza mkono mtoni na kutoa shoka la
               fedha na kumpa Mtema.

                    “Shoka hili si langu,” Mtema alisema.
                   Malaika alilirudisha majini shoka hilo na kutoa majini
               shoka la dhahabu.
                   “Pokea shoka lako,” alimwambia Mtema.
   22   23   24   25   26   27   28   29   30   31   32