Page 25 - Kiswahili Grade 5 Yaliyomo ya kidijitali
P. 25

Na uhuni ukakoma, hekima wakathamini,

                   Ikaingia neema, pembe zote kijijini,
                   Hakika wakaungama, watailinda amani,

                   Na maadili daima, wakatia maanani.


               Shairi 2
                                          Maadili niyaghani








                   Sikio nitegeeni,

                   Shairi nikaririni,
                   Maadili niyaghani.


                   Amani idumisheni,

                   Haki zizingatieni,
                   Na heshima mthamini.


                   Uadilifu chungeni,

                   Umoja kumbatieni,
                   Na upendo upendeni.


                   Usawa hakikisheni,

                   Wajibu utimizeni,

                   Na uzalendo lindeni.
   20   21   22   23   24   25   26   27   28   29   30