Page 23 - Kiswahili Grade 5 Yaliyomo ya kidijitali
P. 23

Sarufi

               Umoja na wingi wa nomino katika ngeli ya U-ZI

               Sikiliza nomino za ngeli ya U-ZI zikisomwa.







                           Umoja                        Wingi
                1.         wimbo                        nyimbo

                2.         wakati                       nyakati
                3.         ufagio                       fagio

                4.         ukuta                        kuta
                5.         ufa                          nyufa

                6.         ulimi                        ndimi
                7.         ufizi                        fizi

                8.         umbavu                       mbavu

                9.         wembe                        nyembe
                10.        waraka                       nyaraka

               Umoja na wingi wa sentensi katika ngeli ya U-ZI

               Sikiliza sentensi zenye nomino za ngeli ya U-ZI zikisomwa.






               1.   Umoja.       Wimbo unasikika vizuri.
                   Wingi.        Nyimbo zinasikika vizuri.

               2.   Umoja.       Wembe unaotumika ni safi na salama.
                   Wingi.        Nyembe zinazotumika ni safi na salama.

               3.   Umoja.       Ufa utazibwa mapema.
                   Wingi.        Nyufa zitazibwa mapema.

               4.   Umoja.       Ukurasa wote unasomeka kwa urahisi.
                   Wingi.        Kurasa zote zinasomeka kwa urahisi.

               5.   Umoja.       Ukwato wa ng’ombe umetibiwa.
                   Wingi.        Kwato za ng’ombe zimetibiwa.
   18   19   20   21   22   23   24   25   26   27   28