Page 20 - Kiswahili Grade 5 Yaliyomo ya kidijitali
P. 20

2.   Juma alianza ufugaji kwa mbuzi mmoja. Alimnunua
                   mbuzi huyo kwa mkopo. Alifanya bidii kumlisha vizuri.
                   Wakati huo huo, alifanya vibarua mashambani mwa

                   wanakijiji. Alilipa mkopo na hata kujiwekea akiba.
                   Polepole, aliwanunua mbuzi wengine wawili. Mbuzi
                   wake walikomaa na kuanza kuzaana. Miaka michache
                   baadaye, Juma aliibukia kuwa mfugaji wa kutajika
                   ndani na nje ya kijiji chao. Watu walitoka mbali na
                   karibu kujifunza kutokana na ufugaji mbuzi wa Juma.
                   Ama kweli, anayejitahidi hufaidi.

               3.   Chuma hakufa moyo kupinga ukiukaji wa haki za
                   watoto kijijini. Aiwashauri wazazi kuwapeleka watoto
                   shuleni. Isitoshe, aliwahimiza waache tabia mbovu za
                   kuwaoza wasichana wao wachanga. Alizunguka kijijini
                   akiwashauri wazazi. Ilikuwa kazi ngumu na yenye
                   hatari lakini aliifanya. Wazazi wengi kijijini walianza
                   kuziheshimu na kuzitetea haki za watoto. Kweli, bidii
                   huleta ushindi.

               4.   Kijiji cha Kwea kilikuwa na shida chungu nzima
                   kutokana na uchafuzi wa mazingira. Chifu wa kata,
                   Bibi Tenda, aliwahamasisha wanakijiji kuyathamini
                   mazingira. Kila siku, alizunguka akiwaelimisha
                   wanakijiji. Alivuka milima na mabonde kuwafikia
                   wanakijiji wengi. Aliwasaidia kuzoa taka na kuzitupa
                   ifaavyo. Wakazi wengi walianza kumuunga mkono.

                   Nao walianza kuwaelimisha wenzao. Polepole,
                   uchafuzi wa mazingira ulitokomea kijijini. Kijiji cha
                   Kwea kikawa safi na mfano wa kuigwa. Kweli, mtaka
                   cha mvunguni sharti ainame.
               5.   Madaktari na wataalamu wa afya hawakufa moyo.
                   Waliongeza bidii katika utafiti wao. Walitumia wakati
                   mrefu na nguvu nyingi kugundua dawa ya ugonjwa

                   huo wa kutisha. Baadaye, walifanikiwa kupata dawa
                   ya kutibu ugonjwa huo. Ama kweli, ukiona vyaelea
                   vimeundwa.
   15   16   17   18   19   20   21   22   23   24   25