Page 16 - Kiswahili Grade 5 Yaliyomo ya kidijitali
P. 16

Kifungu 4

               Soma kifungu kifuatacho.
                                          Siku ya mazingira






















                   Niliamka saa thenashara macheo. Nilijitayarisha kwa

               muda wa saa moja hivi. Mwendo wa saa moja na dakika
               kumi asubuhi, nilianza safari kuelekea eneo ambalo
               lililopangiwa kupandwa miti.
                   Tulifika huko saa moja na nusu asubuhi. Watu
               wachache walikuwa wamefika. Tuliwangoja watu zaidi
               wafike. Baadaye, tulitembea hadi karibu na Mto Rui
               uliokuwa uwekauka. Chifu na wanamazingira wengine

               wangepanda miti kando ya Mto Rui siku hiyo.
                   Tulifika mtoni saa tatu kasoro robo. Tayari chifu na
               watu wengine walikuwa wamefika. Mara moja, shughuli
               zilianza. Sisi hatukupanda miti ila tuliwasaidia tu watu
               wazima kwa shughuli ndogondogo.

                   Shughuli hizo ziliendelea hadi saa nane alasiri.
               Baada ya hotuba fupi ya chifu, kila mtu aliondoka. Watu
               wazima walituongoza hadi sokoni. Tulifika sokoni saa
               tisa alasiri. Tulinunuliwa vyakula na matunda. Baadaye,
               tuliandamana nao hadi nyumbani.

                   Tuliagana na kila mtu akaelekea nyumbani. Nilifika
               nyumbani magharibi. Nilioga na kupumzika. Thenashara
               machweo, nilikula kilalio changu. Baadaye, nilienda
               kulala.
   11   12   13   14   15   16   17   18   19   20   21