Page 17 - Kiswahili Grade 5 Yaliyomo ya kidijitali
P. 17

Mkiwa wawiliwawili, fanyeni shughuli zifuatazo.

               1.   Msimulie mwenzako kisa ulichokisoma kwa ufupi.
               2.   Umejifunza nini kutokana na kisa ulichokisoma?

               3.   Tambueni msamiati mpya kwenye kifungu na uutafutie
                   maana.
               4.   Jitahidi kuutumia  msamiati huo katika mazungumzo
                   yako ya kila siku.

               Sarufi
               Umoja na wingi wa nomino katika ngeli ya I-ZI

               Sikiliza nomino za ngeli ya I-ZI zikisomwa.








                       Umoja                              Wingi
                1.     saa                                saa
                2.     siku                               siku

                3.     sahani                             sahani

                4.     sabuni                             sabuni
                5.     kalamu                             kalamu

                6.     karatasi                           karatasi
                7.     nyumba                             nyumba

                8.     simu                               simu
                9.     nguo                               nguo

                10.    glovu                              glovu
                11.    sindano                            sindano

                12.    dawa                               dawa
                13.    sauti                              sauti

                14.    chati                              chati
                15.    chupa                              chupa
   12   13   14   15   16   17   18   19   20   21   22