Page 13 - Kiswahili Grade 5 Yaliyomo ya kidijitali
P. 13

majilisini. Alibaki hapo hadi saa sita adhuhuri kisha
               mwalimu akamsindikiza hadi kwenye lango la shule.

               Kifungu 2

               Soma matini yafuatayo.
                                              Funzo la Fuai





















                   Fuai alialikwa na Babu Leposo kwa safari. Alifurahi
               kwa sababu alikuwa ameanza likizo. Wawili hawa
               wangeondoka kwa garimoshi la saa mbili na dakika kumi
               asubuhi ya siku iliyofuata. Kituo cha garimoshi hakikuwa
               mbali na nyumbani kwao.

                   “Mimi nitaondoka nyumbani saa moja na robo ili
               nisichelewe,” Babu Leposo alimwambia Fuai.
                   Siku ya safari, Fuai aliamka alfajiri. Alitazama saa na
               kuona ilikuwa saa kumi kamili. Alirudi kulala.

                   Baadaye, aliamka saa mbili kasoro dakika ishirini
               asubuhi. Alijitayarisha chapuchapu. Alifika katika kituo
               cha garimoshi saa mbili na dakika tisa. Milango ya
               garimoshi ilikuwa tayari imefungwa. Garimoshi lililiza
               king’ora cha kuondoka. Fuai alilikodolea macho garimoshi
               huku likiondoka. Alijawa na fedheha.

                   Babu Leposo alirudi nyumbani jioni ya siku hiyo. Fuai
               alinuna alipomuona.
                   “Mbona hungeningoja kwa dakika moja tu?” Fuai
               alimwuliza babu yake.
   8   9   10   11   12   13   14   15   16   17   18