Page 12 - Kiswahili Grade 5 Yaliyomo ya kidijitali
P. 12

Kusoma

               Kusoma kwa mapana: matini ya kidijitali

               Kifungu 1
               Soma kifungu kifuatacho.
                                            Mgeni darasani
















                   Asubuhi hiyo ya Ijumaa ilikuwa ya kipekee kwetu.

               Tulimtarajia mgeni katika darasa letu. Kufikia saa nne
               kasoro dakika ishirini, tulikuwa tumetulia darasani tayari
               kumpokea mgeni wetu.
                   Mgeni alifika saa nne kamili asubuhi. Sote tulisimama
               na kumkaribisha. Alituelezea mengi kuhusu hatua

               za kiusalama wakati wa kutumia vifaa vya kidijitali.
               Alitushauri kila wakati tuyasome matini kutoka tovuti
               salama tu. Alituonya kuwapa watu tusiowajua habari za
               kibinafsi mtandaoni. Habari hizo za kibinafsi ni kama vile:
               majina yetu, majina ya wazazi na walezi wetu na nambari
               zao za simu.
                   Mgeni alitushauri tusiwasiliane na watu tusiowajua
               mtandaoni. Mbali na hayo, alitusihi tusifungue tovuti

               ambazo hatuna uhakika kuzihusu. Aidha, tukiona jambo
               lolote mtandaoni ambalo linatutia wasiwasi, tufunge
               tovuti husika. Vilevile, turipoti jambo hilo kwa mwalimu,
               mzazi, mlezi au mtu mwingine mwenye uwajibikaji.
                   Mgeni wetu alimaliza mazungumzo yake saa tano

               na nusu. Tulimshukuru kwa ushauri wake. Tulimwahidi
               kwamba tungezingatia ushauri huo. Tulimuaga
               akaondoka. Aliandamana na mwalimu wetu hadi
   7   8   9   10   11   12   13   14   15   16   17