Page 14 - Kiswahili Grade 5 Yaliyomo ya kidijitali
P. 14

“Garimoshi lilikuwa na mamia ya abiria. Je, nao
               wangetungoja?” Babu Leposo alimwuliza Fuai.

                   Fuai alipata funzo muhimu tangu siku hiyo. Yeye
               hujitahidi kufanya mambo wakati ufaao.
               Kifungu 3

               Soma kifungu kifuatacho.
                                             Wakati upepo















                   Wanyama wote wa msituni walikuwa wameandaa
               hafla ya kumtuza Mbweha. Mbweha angepewa taji la
               kuwa mnyama aliyeonyesha huruma baada ya kumwokoa
               mtoto wa Sungura alipozama mtoni.

                   Hafla yenyewe ilipangwa kufanyika siku ya Alhamisi.
               Kila mnyama alifaa awe amefika uwanjani saa mbili
               kamili asubuhi. Sherehe zilipangiwa kuendelea hadi saa
               sita adhuhuri.
                   Siku ya hafla, Mbweha alikuwa amepanga kuamka
               alfajiri. Aliamka saa moja na robo asubuhi. Alijitayarisha

               haraka na kuondoka mwendo wa saa moja na nusu.
               Alitimua mbio kuelekea shereheni. Ghafla, aligundua
               hakuwa amebeba kadi ya mwaliko. Lazima angerudi
               kuichukua.
                   Alirudi mbio hadi kwake. Alianza kuitafuta kadi ya

               mwaliko. Hakukumbuka mahali aliiweka. Baadaye,
               aliipata. Alipoangalia saa, ilikuwa ni saa mbili na dakika
               tano asubuhi.
                   Mbweha aliamua kupitia njia ya mkato kwenye
               shamba la Mzee Kiomo. Njia hiyo ilikuwa hatari. Mbweha
               hakujali. Alishika njia ya mkato.
   9   10   11   12   13   14   15   16   17   18   19