Page 5 - Kiswahili Grade 5 Yaliyomo ya kidijitali
P. 5

1.  Mapishi







               Mlango 1. Sherehe Kijijini

               Mlango 2. Baada ya Dhiki Faraja

               Kusikiliza na kuzungumza


               Vitanzandimi
               Sikilizeni vitanzandimi vikikaririwa.






               1.   Tulifurahia vuta nikuvute kati ya mafundi na wavuvi

                   ilipofuatwa na maafikiano badala ya vita.
               2.   Mvulana aliyevaa fulana aliketi kwenye fomu na
                   kukariri silabi za sauti f na v.

               3.   Sisi sote huzima taa zote za sitima tunapoondoka ili
                   nguvu za sitima zisitumike kiholela.
               4.   Mlariba huyo aliharibu sifa kwa kutoza riba ya juu.

               5.   Si siri siku hizi changamoto za maisha zazidi
                   kuongezeka kwa kasi sana.
               6.   Matumizi mazuri ya hela yaliimarisha  ujasiriamali na
                   utekelezaji wa miradi tele ya serikali.

               7.   Askari mlinzi alivaa fulana ya rangi ya buluu na
                   kushika rungu kwa mkono wa kulia.
               8.   Walishirikiana na kuchanga takribani shilingi milioni
                   mbili za kukabiliana na kero lolote la uchafuzi wa
                   mazingira.

               9.   Maria alivaa rinda la rangi ya buluu na blausi ya
                   hudhurungi.

               10.  Walipotuletea redio tusikilize habari kamili, tulifanya
                   maamuzi haraka kabla ya robo saa kuisha wala jambo
                   lolote kutekelezwa.
   1   2   3   4   5   6   7   8   9   10